Simba Mambo Magumu Ligi Kuu, Washindwa Kuipita AZAM, Kagera Sugar Waivuta Shati

  

Simba Mambo Magumu Ligi Kuu, Washindwa Kuipita AZAM, Kagera Sugar Waivuta Shati

Wekundu wa Msimbazi Simba SC imeambulia sare ya 1-1 ugenini dhidi ya Kagera Sugar kwenye muendelezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara


Sare hiyo imewafanya Simba SC kufikisha alama 57 sawa na Azam FC wakisalia kwenye nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo nyuma ya Azam FC wenye wastani mzuri wa magoli ya kufunga na kufungwa.


Simba SC watajilaumu wenyewe kwa kukosa nafasi za wazi kwenye mchezo huo kupitia kwa mshambuliaji wake Fred aliyekosa nafasi 3 za wazi.


Sasa michezo minne imesalia kutamatisha ligi hiyo ambayo kama Azam FC wataitumia vizuri basi watajihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya klabu bingwa Afrika msimu ujao.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad