Celine Dion Japo Bado Mgonjwa Adai Atarudi Jukwaani Hata Kwa Kutambaa

 

Celine Dion Japo Bado Mgonjwa Adai Atarudi Jukwaani Hata Kwa Kutambaa

Mwanamuziki mkongwe na maarufu duniani kutokea nchini Canada, Celine Dion amesema hataruhusu vita vyake na ugonjwa unaomsumbua wa (Stiff Person Syndrome) kumzuia kufanya maonyesho ya muziki.


Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 56, aliyasema hayo kwenye mahojiano na Hoda Kotb na kuapa kwamba ataendelea kufanya maonyesho hata kama atalazimika kutambaa kwenye jukwaa na kuzungumza kwa mikono.


“Nitarudi kwenye kwenye stage, hata ikiwa ni lazima nitambae. Hata ikibidi nizungumze kwa mikono,, nitafanya”.


Mwanamuziki huyo amekuwa akipambana kwa siri na ugonjwa huo unaomsumbua kwa miaka 17, kabla hajaamua kuweka wazi mwaka juzi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad