GSM, Bakhresa, Mo Enterprises Wajitosa Kuwekeza Treni ya SGR



Dar es Salaam. Kampuni sita za Kitanzania ni miongoni mwa kampuni kadhaa ambazo zimeonyesha nia ya kushirikiana na serikali katika kuendesha Reli ya Standard Gauge (SGR).

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa kufuatia kutangazwa kwa Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka 2024.

Akizungumza na Mwananchi leo Juni 19, 2024, Kadogosa amezitaja kampuni hizo kuwa ni GSM, Bakhresa Group, Mohammed Enterprises Company Limited, Lake Oil, Azania na Jambo.

Orodha hiyo pia inajumuisha kampuni kadhaa kutoka China na Ulaya.

“Kati ya kampuni zilizotajwa hapo juu, Jambo ndiyo kampuni pekee ya Kitanzania ambayo imeonyesha nia ya kuanzisha treni ya kifahari ya abiria kwa ajili ya watalii. Asilimia 99 iliyobaki wana hamu ya kuwekeza kwenye usafirishaji wa mizigo,” amesema.

Amesema kwa sasa TRC inajitahidi sana kuhakikisha ujenzi wa sehemu zote za SGR unakamilika ifikapo 2028 ili wawekezaji watumie fursa hiyo na kutoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi.

Hata hivyo, amesisitiza kwamba SGR siyo mbadala wa mabasi ya mikoani, malori, ndege na reli ya kawaida (MGR) lakini alibainisha kuwa zote zinakusudiwa kusaidia na kupanua sekta ya uchukuzi.

Alisema uendelevu wa SGR unategemea matengenezo ndiyo maana Watanzania na wawekezaji walitakiwa kulipia huduma hiyo ili kuitunza.


"Tusipofanya hivyo, hatutakuwa na SGR baada ya miaka kadhaa...SGR hii imejengwa kuweza kuishi kwa muda wa miaka 100, ni muhimu kuitunza,” amesema.

Wakati huohuo, Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za 2024, zinazoruhusu ubia katika uendeshaji wa reli kati ya Serikali na sekta binafsi, zimechapishwa kwenye gazeti la serikali.

“Tulitangaza kwenye kanuni hizo katika gazeti la serikali Namba 213, Machi 29, 2024. Mambo mengi ambayo yalipendekezwa katika ufikiaji huo hayajabadilika sana, kunaweza kuwa na mabadiliko kidogo. Lakini ikiwa kuna mabadiliko lazima yawe machache sana,” amesema Kaimu Mkuu wa Huduma za Kisheria katika Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu (Latra), Mwadawa Sultan.


Ameiambia Mwananchi kuwa Latra ilihusisha wadau tangu mwanzo wa utungaji wa Kanuni za Matumizi ya Reli za mwaka 2024 ambao walikuja na maoni kadhaa muhimu yaliyosaidia kuboresha hati asili.

Chini ya kanuni hizo za 2024, wanaotaka kuwa waendeshaji huru wa reli, watalazimika kutimiza mahitaji kadhaa, ikiwa ni pamoja na kutuma maombi rasmi na kutoza gharama ipasavyo.

“Tulitangaza katika Kanuni za Matumizi ya Reli katika gazeti la serikali Namba 213, Machi 29, 2024. Mambo mengi ambayo yalipendekezwa katika kanuni hizo hayajabadilika sana, kunaweza kuwa na mabadiliko kidogo. Lakini kama kuna mabadiliko, ni machache sana,” alisema Kaimu Mkuu wa Huduma za Kisheria katika Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu (Latra), Mwadawa Sultan.

Ameiambia Mwananchi kuwa Latra ilihusisha wadau tangu mwanzo wa utungaji wa Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka 2024, ambao walikuja na maoni kadhaa muhimu ambayo yalisaidia kuboresha hati asili.

Chini ya Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka 2024, wale wanaotaka kuwa waendeshaji huru wa reli watalazimika kutimiza mahitaji kadhaa, ikiwa ni pamoja na kutuma maombi rasmi na kutoza gharama ipasavyo.

Baada ya kutuma maombi na kupewa leseni na ofisa wa serikali anayejulikana katika kanuni kama Meneja wa Miundombinu, mwendeshaji atapewa kibali na haki za usafirishaji kwa madhumuni ya kufanya kazi kwenye aina yoyote ya reli.

Waendeshaji watalazimika kulipa ada ya maombi na ada ya leseni.

Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka 2024 zinaonyesha kuwa waombaji watalipa leseni na ada ya maombi ya Dola za Marekani 2,000 na dola 100 kwa huduma za abiria.

Kwenye mizigo, waombaji watalipa leseni na ada ya maombi ya dola100 na dola 4,000.

Akizungumza Oktoba, mwaka jana wakati wa kikao cha kujadili kanuni hizo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk Ally Posi alisema fedha zitakazolipwa na waendeshaji hao binafsi zitatumika kimsingi kwa matengenezo ya reli.

Alisema ni vema kushirikisha sekta binafsi katika uendeshaji wa njia ya reli, ikizingatiwa kuwa kipimo cha reli ya kawaida kinafanya kazi chini ya uwezo wake.

“Sote tunajua miundombinu ya reli ya kawaida (MGR) ilitengenezwa kubeba mizigo ya tani milioni tano kwa mwaka lakini shehena kubwa inayosafirishwa hadi sasa ni tani milioni 1.6. Kwa hivyo, tuna upungufu wa karibu tani milioni 3.4,” alisema Dk Possi, Oktoba mwaka jana.

“Kwa kuwa ujenzi wa SGR unaendelea vizuri, ushiriki wa sekta ya kibinafsi katika uendeshaji wake hauhitaji kutiliwa mkazo kupita kiasi,” aliongeza.

Dk Possi alisema uwekezaji zaidi kutoka sekta binafsi utahitajika ili serikali itambue manufaa ya fedha zinazoingizwa kwenye mradi huo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad