Kimenuka Simba! Viongozi WOTE wadaiwa kujiuzulu, Try Again agoma

 

Kimenuka Simba! Viongozi WOTE wadaiwa kujiuzulu, Try Again agoma

Wakati Mashabiki wa Simba wakiwa bado wana shauku ya kutaka kujua Timu yao ina mpango gani kuelekea msimu mpya 2024/25 baada ya kutokuwa na msimu mzuri 2023/24.


Waandishi wa Habari nguli kutoka nchini wamekuja na taarifa inayoonesha hali si shwari katika Klabu ya Simba.


Mwandishi wa Habari ktoka Clouds FM, Shaffih Dauda ameandika;


Taarifa kutoka kwenye chanzo cha kuaminika ni kwamba wajumbe wote wa bodi ya klabu ya @SimbaSCTanzaniakutokea upande wa mwekezaji @moodewji wamejiuzulu!


Bodi ya Wakurugenzi wa Simba inaongozwa na Mwenyekiti Salim Abdallah Muhene "Try Again"


Wakati Taarifa zikieleza hayo Mwandishi wa Habari Kutoka Kituo cha E-Fm Jemedari Said kupitia kurasa zake za mitandao ya Kijamii ameandika;


"Mwekezaji wa Simba SC mwenye 49% Mohamed DEWJI amewapigia simu wajumbe wa Bodi ya klabu ambao wanatokana na upande wake (aliowateua yeye) na kuwataka wajiuzulu nafasi zao. Mpaka sasa wajumbe 3 wamegoma kutii AMRI ya tajiri ambao ni RASHIDI SHANGAZI,HAMZA JOHARI NA SALIM ABDALLAH

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad