Yanga Ruksa Kusajili, Walipa Madeni Yao Yote.....


Yanga Ruksa Kusajili, Walipa Madeni Yao Yote.....

Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limeiondolea Young Africans adhabu ya kufungiwa kusajili wachezaji baada ya kukamilisha malipo ya aliyekuwa mchezaji wao Lazarus Kambole.

Awali, mchezaji huyo raia wa Zambia alifungua kesi FIFA dhidi ya klabu hiyo ya Ligi Kuu ya NBC kwa kushindwa kumlipa ujira wake. Kambole alishinda kesi hiyo, na Young Africans ilitakiwa kumlipa ndani ya siku 45 tangu uamuzi huo wa FIFA ulipotolewa, lakini haikutekeleza uamuzi huo na kusababisha ifungiwe kusajili.

Baada ya kukamilisha malipo hayo, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) nalo limeifungulia Young Africans kufanya uhamisho wa ndani wa wachezaji.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad