Mbrazil Robertinho Kuwa Kocha Klabu ya Rayon Sports ya Rwanda



Klabu ya Rayon Sports ya Rwanda imemtangaza aliyekuwa Kocha wa Simba SC mbrazil Robertinho kuwa Kocha mkuu klabuni hapo.

Robertinho anarejea klabuni hapo baada ya awali kuiongoza Rayon Sports kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Rwanda mnamo mwaka 2019.

“Tunayo furaha kutangaza kwamba mkufunzi wa Kimataifa wa Brazil Roberto Oliveira Goncalves do Carmo, anayejulikana kama “ROBERTINHO” ameteuliwa kuwa Kocha wetu Mkuu,” imesema taarifa ya klabu hiyo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad