Pacome Ameomba Kuondoka Yanga - Oruma Afunguka

 
Pacome Ameomba Kuondoka Yanga - Oruma Afunguka


Wilson Oruma kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

"Hizi inaweza kuwa taarifa kubwa zaidi hapa Tanzania kwenye dirisha hili Kubwa la Usajili 2024.

"Taarifa za uhakika kutoka kwenye chanzo changu zinadai Pacome Zouzoua amepata offer kubwa kutoka kwa Mabingwa wa Africa, Al Ahly.

"Kumbuka Pacome Zouzoua Peodoh amebakisha mwaka mmoja kwenye mkataba wake na Young Afrika SC hivyo amewaambia ni bora Kumuuza sasa kuepusha hatari ya Kuondoka bure msimu ujao kwasababu hana mpango wa Kuongeza Mkataba mpya.

Mchambuzi Dominick Salamba anajibu;

"Pacome is staying
Klabu alizozichomolea mpaka sasa:
Azam FC
FAR Rabat
Kaizer Chiefs.

Mpaka sasa Zidane wa Africa 'Paccome ZouZoua' amefikia makubaliano ya kuongeza mkataba ulioboreshwa vipengele vya maslahi binafsi ndani ya Yanga SC.

Mkataba wa miaka miwili - Uko mezani.
Mshahara ulioboreshwa - Uko mezani.
Aidha mchezaji huyo ameueleza uongozi kuwa anafurahia mazingira yake ya kazi na utulivu ulioko nchini.

Sio tu kuongeza mkataba, anaweza hata kununua kiwanja na kuanza ujenzi akiwa Bongo.

Mnasemaje hapa?"

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad