Shaffih Dauda "Nimependa usajili wa Yanga"

Shaffih Dauda "Nimependa usajili wa Yanga"


Mchambuzi wa masuala ya Soka kupitia Clouds FM kipindi Hili Game, Shaffih Dauda amesema kuwa amependa aina ya usajili wa wanaoufanya Yanga na kuwabakisha nyota wake wake muhimu.


Dauda amesema hayo baada ya Yanga kumsajili aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Simba, Clatous Chama huku kukiwa na tetesi za kumsajili mshambuliaji Prince Dube ambaye ameshavunja mkataba wake na Azam FC.


“Nimependa namna Yanga wanavyosajili, wachezaji wao muhimu wote wamefanikiwa kuwabakisha, bila shaka hawa wachezaji wameonesha uwezo mkubwa sana mtu kama Aucho haimbwi vile inavyotakiwa lakini ameonesha kiwango cha juu sana.


“Tumezoea kuwaimba wachezaji wanaofunga tu , tuzo za mwezi wanapewa wafungaji Aucho anaathirika kwa mentality hiyo ambayo atazungumzwa zaidi Aziz Ki , Feisal ambao wanafunga magoli,” amesema Shaffih Dauda.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad