Fei Toto na Yanga Bado Damu Damu, Wakumbatiana na Eng Hersi

Fei Toto na Yanga Bado Damu Damu, Wakumbatiana na Eng Hersi


Wakati kikosi cha Azam FC inakwenda kuchukua medali ya mshindi wa pili wa michuano ya Ngao ya Jamii, kama kuna tukio kilikuwa linasubiriwa basi ni kiungo Feisal Salum Fei Toto kuonana uso kwa uso na Rais wa Yanga injinia Hersi Said na wamekutana bana.


Katika zoezi hilo la kupokea medali Fei Toto amekutana na Hersi ambaye alikuwa jukwaa la viongozi walioshiriki kutoa zawadi ambapo  kwa mara ya kwanza wakakutana.


Hata hivyo, Fei Toto hakuwa na shida na mtu, akasalimiana na Hersi kwa kupeana mikono kisha wawili hao kukumbatiana na kuongea kwa sekunde chache.


Wakati wakisalimiana na kukumbatiana mashabiki wa Yanga wakalipuka kwa furaha wakishangilia  kwa nguvu, huku Fei akiondoka na medali akiwa ameivaa kisha kuivua baada ya mwendo mfupi.


Awali Fei Toto wakati anaondoka Yanga aliwahi kukaririwa akisema hata rejea timu hiyo endapo Hersi atakuwa Rais wa klabu hiyo. Tangu ameondoka Yanga Fei Toto ameshawafunga waajiri wake wa zamani mabao matatu kwenye mechi tofauti za mashindano.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad