Mchango wa Simba Kutoa Wachezaji Timu ya Taifa Umepungua

 

Mchango wa Simba Kutoa Wachezaji Timu ya Taifa Umepungua

Kocha wa Taifa Stars, Hemed Morocco ametaja kikosi kitakachojiandaa na mechi za kufuzu Afcon.

Katika orodha ya majina Klabu ya Yanga imetoa wachezaji saba,,Azam wachezaji watano na Simba imetoa wachezaji watatu tu.

Takwimu hizi zinathibitisha kuwa kwa miaka ya karibuni Klabu ya Simba imepunguza mchango wake kwenye kikosi cha Taifa Stars tofauti na miaka mitano iliyopita ambapo ilishuhudiwa mnyama akitoa wachezaji kuanzia sita na kuendelea.

Enzi za ubora wake Simba ndio Klabu iliyokua ikisifika kwa kuwa na wachezaji bora wazawa nchini wakiwemo Aishi Manula,Shomari Kapombe,John Bocco,Erasto Nyoni,Jonas Mkude,Mzamiru Yassin,Kennedy Juma ambao wote hawa hawapo kwa sasa ingawa uwakilishi uliotukuka unasalia kwa Mohamed Hussein Zimbwe Jr aliyepo hadi sasa.

Orodha ya majina .

YANGA

Aboutwali Mshery

Dickson Job

Ibrahim Bacca

Bakari Nondo

Mudathir Yahya

Nickson Kibabage

Clement Mzize

AZAM

Feisal Salum

Adolf Mtasingwa

Pascal Msindo

Nathaniel Chilambo

Lusajo Mwaikenda

SIMBA

Ally Salim

Edwin Balua

Zimbwe Jr

Nyakati zinasogea!ndio maana kwa sasa Simba inapambana kusajili wachezaji vijana wa ndani wakiwemo Valentino Mashaka,Kelvin Kijiri nk ili kurejesha utawala wao!

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad