Simba Waifanya Haya Watakuwa Tayari Kupigania Ubingwa wa Msimu ujao


Binafsi kama Hans Rafael sioni haja ya Simba kubaki na magolikipa wawili wa kigeni,huu ni uharibifu wa nafasi za wachezaji wa kigeni.

Nadhani Simba wanatakiwa kubaki na Camara kama kipa namba moja huku akisaidiwa na Ally Salim na Abel,kisha waachane na Ayoub ambae hayuko fit.

Wakati huo Simba waachane na Freddy ambaye haingii kwenye mfumo wa Fadlu kisha waingie sokoni kupata namba 9 wa maana na winga mmoja wa kulia mwenye kasi na ujuzi wa kufunga magoli mfano yule Derrick Fordjour wa Medeama anafaa sana.

Baada ya hapo Simba watakuwa tayari kupigania ubingwa wa msimu ujao✍️

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad