Tundu Lissu, John Mnyika, Sugu Wakamatwa Mbeya

  

Tundu Lissu, John Mnyika, Sugu Wakamatwa Mbeya

Polisi Mkoani Mbeya wamewakamata Watu wote waliokuwa Ofisi za CHADEMA Kanda ya Nyasa akiwemo Makamu Mwenyekiti CHADEMA Bara Tundu Lissu, Katibu Mkuu John Mnyika na Mwenyekiti wa Kanda Joseph Mbilinyi (SUGU) leo August 11,2024.


Lissu, Mnyika na Sugu wamewasili Mbeya saa kadhaa leo ili kuungana na Vijana wa Chama hicho kupitia Baraza la Vijana CHADEMA ( BAVICHA) waliokua wameandaa maadhimisho ya siku ya Vijana Duniani.


John Mrema ambaye ni Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje - CHADEMA, amethibisha kukamatwa kwa Viongozi hao pamoja na wengine kutoka Baraza la Vijana BAVICHA.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad