BODI YA LIGI YAKATI MZIZI WA FITINA: KAGOMA NI MCHEZAJI HALALI WA SIMBA



BODI ya Ligi imesema inamtambua Yusuph Kagoma kuwa ni mchezaji halali wa Simba kwani ana leseni ambayo imetoka kwenye mamlaka ya Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), ambao ndiyo wanaowaletea majina na leseni zao kuthibitisha kuwa wako halali na wanaruhusiwa kutumika kwa timu husika.

Ofisa Habari wa Bodi ya Ligi, Karim Boimanda, amesema changamoto kwao kama Bodi ya Ligi ingekuwa kama wamemruhusu mchezaji huyo kucheza bila ya kuwa na leseni, lakini kwa sababu anayo na inamtaja kuwa ni mchezaji wa Simba, basi ana uhalali wote wa kuichezea timu hiyo.

Amebainisha Simba haiwezi kupokwa pointi kwa kumchezesha mchezaji huyo katika michezo yake ya ligi kwa sababu anacheza akiwa amekamilisha taratibu zote, na migogoro yote huwa inatatuliwa kwenye Kamati za TFF, kabla ya wao kuletewa maamuzi yakiwa yamekamilika.

Boimbanda alisema hayo kufuatia utata uliozuka hivi karibuni kwa Klabu ya Yanga, kudai ina mkataba wa miaka mitatu na Kagoma ambaye wanashangaa kuona amesajiliwa pia na Simba, wakisema kitendo hicho kinaonesha kuwa amesajili timu mbili.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad