DENIS NKANE NA SOPU WAPEWE NAFASI KUONESHA VIPAJI VYAO....KICHUYA


Licha ya wachezaji Denis Nkane kukosa namba kwenye kikosi cha Yanga kutokana na uwepo wa mawinga wa kigeni wanaofanya vizuri, Kichuya amemkingia kifua na akimtaja kuwa ni mchezaji mzuri anatakiwa kupewa nafasi ili aonyeshe.

“Nkane ni winga mzuri sana na sio huyo tu kwa upande wa wazawa eneo hilo tupo vizuri kuna Iddy Nado na Abdallah Suleiman ‘Sopu’ wote wana uwezo mkubwa na wakipewa nafasi watafanya mambo makubwa kama ilivyo kwa Feisal Salum ‘Fei Toto’ ambaye ameonyesha changamoto akitupia mabao mengi kuzidi washambuliaji,” anasema winga huyo.

“Kila msimu kunaibuka vipaji vipya na kuna vingine vinakosa kuonyesha uwezo wao kutokana na uwepo wa wachezaji wa kigeni ambao wengine hata hawana uwezo lakini kutokana na gharama kubwa wanazopewa wanalazimika kutumiwa tu.”

Anasema hana maana kwamba wachezaji wanaocheza eneo la wingi wote hawana uwezo kuna wengine wamekuwa chachu ya kupandisha uwezo wa wengine lakini anatamani kuona wachezaji wazawa pia wanapewa kipaumbele ili waonyeshe uwezo walionao.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad