SIRI YA CHAMA KUCHEZA ZAIDI TIMU YA TAIFA YA ZAMBIA BAADA YA KUJIUNGA YANGA

SIRI YA CHAMA KUCHEZA ZAIDI TIMU YA TAIFA YA ZAMBIA BAADA YA KUJIUNGA YANGA

 Siri ya Chama kucheza zaidi Chipolopolo akiwa na Yanga« NyumaMbele »Comments (0)Listen to Article

 

Kumekuwa na mijadala mingi sana mitandaoni kuhusu nafasi ya Clatous Chama kwenye timu ya taifa ya Zambia, kwa sasa akiwa Yanga na wakati akiwa Simba.


Wanatakwimu wa mitandaoni wanasema tangu ahamie Yanga kwenye dirisha kubwa la usajili lililopita, Chama amekuwa akipata sana nafasi zaidi kwenye kikosi cha Chipolopolo, kuliko wakati ule akiwa Simba SC.


Ukurasa huu umejaribu kufanya utafiti wa mchezaji huyo kwenye timu ya taifa, katika kipindi hiki yuko Yanga kwa kulinganisha na kipindi kile akiwa Simba.


Utafiti huu umeangalia mechi zote za timu ya taifa ya Zambia za mwaka 2024, ambao umemgawa Chama mara mbili, akiwa Simba na akiwa Yanga.


1. Akiwa Simba


Wakati mwaka 2024 unaanza, Chama alikuwa mchezaji wa Simba, na aliendelea kuwa mchezaji wa Simba hadi Juni 30 mwaka huu mkataba wake ulipoisha.


Katika kipindi hicho, Zambia ilicheza mechi 10, za mashindano rasmi na za kirafiki.


MECHI


MASHINDANO


TAREHE


KUCHEZA


MCHANGO


Zambia 1-1 Cameroon


Kirafiki


09/01/2024


Alikuwa benchi


DR Congo 1-1 Zambia


AFCON


17/01/2024


Alikuwa benchi


Zambia 1-1 Tanzania


AFCON


21/01/2024


Aliingia dk 76


Asisti


Zambia 0-1 Morocco


AFCON


24/01/2024


Aliingia dk 83


Zambia 2-2 Zimbabwe


Kirafiki


23/03/2024


Alicheza dk 90


-Bao 1


Zambia 2-1 Malawi


Kirafiki


26/03/2024


Aliingia dk 64


-Bao 1 na asisti


Morocco 2-1 Zambia


Kufuzu WC


07/06/2024


Hakuitwa


-


Zambia 0-1 Tanzania


Kufuzu WC


11/06/2024


Hakuitwa


-


Zambia 0-2 Kenya


COSAFA


27/06/2024


Hakuitwa


Zambia 0-2 Zimbabwe


COSAFA


30/06/2024


Hakuitwa


NB: Timu alicheza mechi nne na kutumia jumla ya dakika 313 katika sita alizoitwa kati ya 10 ambazo Zambia ilicheza. Katika sita alizoitwa, alifanikiwa kucheza katika mechi nne.


2. Akiwa Yanga


Alfajiri ya Julai mosi, 2024 Yanga waliposti picha ya Clatous Chama akisaini kuitumikia klabu hiyo na kuthibitisha tetesi za muda mrefu.


Mkataba wake ukaanza kuwa rasmi tangu siku hiyo.


Katika kipindi hicho, Zambia imecheza mechi tatu tu, kama ifuatavyo.


MECHI


MASHINDANO


TAREHE


KUCHEZA


MCHANGO


Comoro 1-0 Zambia


COSAFA


02/07/2024


-Hakuitwa


-


Ivory Coast 2-0 Zambia


Kufuzu AFCON


06/09/2024


-Alicheza dk 64


-


Zambia 3-2 Sierra Leone


Kufuzu AFCON


10/09/2024


-Alicheza dk 89


-


NB: Katika kipindi akiwa Yanga, Zambia imecheza mechi tatu tu huku yeye akiitwa katika mechi mbili katika hizo na akicheza jumla ya dakika 153.


Japo dakika zinaweza kuonekana chache akiwa Yanga kuliko alipokuwa Simba, lakini kiuhalisia huku ndiyo amefaidi zaidi kuwepo timu ya taifa kuliko wakati ule.


CH4 CH4


Hii ni kwa sababu wastani wa mechi na dakika ni mzuri zaidi kuliko kule. Hapa ndipo wachambuzi wa Tanzania wanaposhadadia wakisema anapata zaidi muda wakati huu kwa sababu yuko Yanga.


Lakini hiyo siyo kweli, ni mambo tu ya kishabiki, ukweli ni kwamba Chama anapata zaidi muda wakati huu kutokana na kushuka kwa viwango vya watu waliokuwa wakimuweka benchi wakati ule.


Wale wachezaji waliokuwa wanaanza mbele ya Chama wakati ule, sasa hivi hawana kitu kabisa. Wakati ule nafasi ya Chama kwenye kikosi cha Zambia ilikuwa ngumu sana kutokana na watu aliokuwa anashindana nao katika nafasi ambazo yeye anaweza kucheza.


Nafasi zote ambazo Chama anaweza kucheza zilikuwa na wachezaji waliomzidi uwezo. Nitakuchambulia nafasi moja moja.


CH5 CH5


Namba 10


Hii ndiyo nafasi ambayo Chama huwa anaimudu vizuri kuliko zote, na anaifurahia sana kucheza.


Lakini wakati ule kwenye timu ya taifa ya Zambia nafasi hii ilikuwa ikimilikiwa na Fashion Sakala, nyota wa klabu ya Rangers ya Scotland.


Msimu uliopita wakati akimsugulisha benchi Chama kwenye timu ya taifa, Sakala alimaliza akiwa amefunga mabao 10+ na kutoa asisti 10+ za mabao kwenye ligi yao.


Hakuna kocha anayetaka ushindi atamuacha mtu kama huyu nje ilhali ni mzima wa afya, halafu akamuanzisha Chama. Labda kama kuna matatizo ya kiufundi au kinidhamu.


Lakini sasa Sakala siyo yule tena na mara kadhaa nafasi hii imekuwa ikitawaliwa na Edward Chilufya wa klabu ya Midtjylland ya Denmark.


Kwenye mchezo wa kipigo cha 2-0 kutoka Ivory Coast, Chama aliingia dakika ya 26 kuchukua nafasi ya huyu.


Namba 8


Nafasi nyingine ambayo Chama anaweza kucheza, angalau kwa kulazimisha, ni namba nane. Lakini kwa bahati mbaya kwenye kikosi cha Zambia wakati ule nafasi hii ilikuwa mali ya Kings Kangwa anachezea Belgrade Red Star ya Serbia.


Kwenye ligi yao jamaa alifunga mabao 10+ msimu uliopita, wakati akimsugulisha Chama.


Mwezi Machi mwaka jana, Kangwa alimpisha Chama katika dakika ya 81 kwenye mchezo wa kiraki dhidi ya Malawi.


Jamaa bado kaishikilia nafasi hii na Chama hajathubutu kabisa kuchukua nafasi yake hata kwa sekunde.


Winga namba 7


Labda tuseme kocha ajilipue na kumpanga Chama kama winga wa kulia. Lakini hata hivyo, kwa Zambia hilo haliwezekani kwa sasa kama ambavyo lilikuwa haliwezekani wakati ule kwa sababu nafasi hii ni mali ya Emmanuel Banda kutoka Rijeka ya Croatia.


Jamaa ana kasi, nguvu na maarifa yanayoweza kumshawishi kocha yoyote kumpa nafasi.


Winga namba 11


Mara kadhaa klabuni Simba wakati ule Chama alikuwa akicheza kama winga wa kushoto ili kutoa nafasi kwa timu kuanza na washambuliaji pacha (wakati wa Bocco na Kagere) au hata baadaye kuruhusu yeye na Saido Ntibazonkiza kuanza pamoja.


Lakini hilo halikuwezekana wakati ule akiwa Simba hata sasa akiwa Yanga kwa timu ya taifa ya Zambia kwa sababu nafasi hii ni mali ya Lameck Banda wa Lecce ya Italia.


Kwa hiyo licha ya umaarufu wake hapa nyumbani na hata kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, bado Chama aliendelea kuchoma mahindi kwenye timu ya taifa.


Lakini sasa, kuyumba kidogo kwa Fashion Sakala kunaweza kumrahishia kazi Chama na kuendelea kutamba zaidi na timu ya taifa.


Lakini sababu siyo kwamba yuko Yanga, hapana, ni kiushuka kwa viwango kwa wale waliokuwa wakimchomesha mahindi wakati ule pale Chipolopolo.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad