Imegundulika Kimbe Mwanamuziki Liam Payne Alitemwa na Lebal yake Kabla ya Kufariki...

Imegundulika Kimbe Mwanamuziki Liam Payne Alitemwa na Lebal yake Kabla ya Kufariki...

Msanii wa zamani wa One Direction, Liam Payne, ameripotiwa kufariki kwa kuanguka kutoka gorofa la tatu katika hoteli ya CasaSur Palermo, Buenos Aires, Argentina. Tukio hilo lilitokea Jumatano jioni huku Payne akiwa amekuwa na tabia ya kuharibu vyumba vya hoteli na kufanya vitendo vya utata kabla ya kifo chake.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, Universal Music walimfuta Liam Payne kwenye orodha yao ya wasanii siku chache kabla ya tukio hilo kutokana na changamoto za muziki wake, ambao ulikuwa hauendelei vizuri. Uvumi wa changamoto za kisheria na matatizo ya mahusiano yake na mpenzi wake wa zamani, Maya Henry, ziliongeza shinikizo kwa msanii huyo kuwa na tabia za ajabu, Liam pia alisemekana kuwa na changamoto za afya ya akili.

Universal Music ilitoa salamu za rambirambi, ikisema kuwa "urithi wake utaendelea kuishi kupitia muziki wake na mashabiki wengi aliowatumikia."

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad