Mchezaji Philipe Kinzubi Kutoa SIMBA, Eng Hersi Aliambulia Kupiga Nae Picha tu


Mchezaji Philipe Kinzubi Kutoa SIMBA, Eng Hersi Aliambulia Kupiga Nae Picha tu

Club Africaine ya nchini Tunisia imekubali kumuachia winga mshambuliaji hatari Raia wa DRC CONGO PHILIPE KINZUMBI mwenye umri wa miaka 25 ambaye ameomba kuondoka katika timu hiyo dirisha dogo la usajili linalofunguliwa tarehe 15 mwezi wa 12 na kufungwa tarehe 15 mwezi january na taarifa kutoka kwa wakala anayemsimamia mchezaji huyo amesema kituo kinachofuata ni Msimbazi kariakoo timu ambayo imekuwa ni chaguo lake na ndoto yake ya muda mrefu sana tangu alivyoanza kucheza soka la kulipwa.

Hapo awali uongozi wa Yanga ulifanya kila linalowezekana ili kuipata saini ya mchezaji huyo hadi Rais wa Yanga alisafiri kwenda hadi Nchini DR Congo akakutana na Rais wa timu ya TP Mazembe Moise Katumbi kujadili uhamisho wa mchezaji huyo jambo ambalo lilishindikana kwakuwa mchezaji huyo alikataa kujiunga na Yanga kutokana na offer kubwa iliyokuja mezani kutoka kwa Raja Cassablanca kisha Rais wa yanga akaambulia kupiga tu picha na Rais wa Tp Mazembe na kisha kurejea nchini.

Mara baada ya dili la kutua Raja Cassablanca kuleta gagaziko basi mchezaji huyo alitua rasmi Club Africaine ambapo yupo hadi hivi sasa, mara baada ya Timu hiyo yake ya sasa kuridhia kuondoka kwa mshambuliaji huyo hatari kwenye eneo la winga basi uongozi unaomsimamia mchezaji huyo umefanya jitihada za kutimiza ndoto za kujiunga na msibazi na kila kitu kimekwenda vizuri kinachosubiriwa ni muda tu kijana kutua rasmi ndani ya mitaa ya msimbazi na uhuru kariakoo

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad