Ruben Dias: Rodri Hernández Anastahili Tuzo ya Ballon D'or

 

Rodri Hernandez

Wakati wengi wakiamini kuwa mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid Vinicius Jr kutwaa tuzo ya Ballon D'or itakayotolewa kesho Jumatatu, beki wa kati wa klabu ya Manchester City Ruben Dias amekomaa na kusema kuwa kiungo wa kati wa klabu hiyo Rodri anastahili kutwaa tuzo hiyo.


Ruben Dias amempigia chapuo Mhispaniola mwenzake ambaye msimu uliomalizika alishinda taji la Euro, Ligi kuu Uingereza huku Vinicius akibeba taji la UEFA Champions league na ligi kuu Hispania.


Rodri na Vinicius wanatajwa kuwa washindani wakuu wa tuzo hizo msimu huu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad