Yanga imerejea katika usukani wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kishindo baada ya kuifunga Timu ya KenGold kwa Magoli 6-1 kwenye Uwanja wa KMC, hivyo kuongoza msimao wa Ligi kwa kufikisha alama 45
-
Magoli ya #Yanga yamefungwa na Prince Dube dakika ya 1 na 46, Clement Mzize (5 na 42), Pacome Zouzoua (38) na Duke Abuya (85) wakati lile la #KenGoldFC mfungaji ni Selemani Bwenzi (86) aliyefunga kwa kupiga shuti kutoka katikati ya uwanja
-
Yanga imecheza michezo 17 imeishusha Simba yenye alama 43 ikiwa na michezo 16, wakati KenGold imebaki mkiani ikiwa na alama 6 katika michezo 17