Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeuruhusu uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam kutumika kwa michezo ya robo fainali na nusu fainali Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF CL) na Kombe la Shirikisho Afrika (CAF CC) 2024/2025.
Uwanja huo umeruhusiwa baada ya Ukaguzi uliofanywa na Wakaguzi wa CAF hivi karibuni.
CAF inaendelea kufuatilia kwa karibu maboresho yanayoendelea kwenye uwanja huo.