Nimesoma vizuri barua ya Simba Ila kuna ÅŸehemu Kama mbili wameniacha njia panda.
1. “Katika Sintofahamu hiyo, Simba iliarifiwa na Meneja wa Uwanja kuwa hana maelekezo ya kuruhusu mazoezi kufanyika bila maelekezo ya kamishna wa Mchezo”
Kupitia huu mstari ni wazi Simba hawajazuiliwa na mabaunsa kuingia uwanjani bali wamezuiliwa na meneja wa uwanja kwani ndie mwenye mamlaka na funguo Za kuruhusu watu waingie uwanuani.
2. “Mabaunsa wa Klabu ya Yanga walivamia Msafara wa Simba huku wakiendelea na vurugu na wakizua Msafara wa simba kuingia uwanjani kufanya mazoezi”
Kwenye mstari mwingine Simba wameandika juu ya Mabaunsa wa Yanga,binafsi hapa wameniacha njia panda,najiuliza Wamejuaje kama wale ni Baunsa wa Yanga? Mbaya zaidi kwenye lile eneo hakukuwa na kiongozi yeyote wa Yanga Sasa wao wamejuaje kama wale ni Baunsa Wa Yanga? Au walikuwa na jezi au vitambulisho vya Yanga?maana viongozi wote wa Yanga wamesajiliwa TFF hakuna sehemu Yanga wamesajili Baunsa.
Lakini pia Barua ya Simba inasema Baunsa wa Yanga wameizuia timu kuingia ndani,ila ukiangalia video za lile tukio Baunsa walikuwa nje ya uwanja,ina maana na wao hawakuwa na mamlaka ya kuingia ndani kwani meneja Wa uwanja alitia Rock,pia tujiulize swali Mabaunsa ambao walikuwa nje wanaweza vipi kumzuia mtu asiingie ndani wakati uwanja umefungwa?
Hii barua ya Simba ina maswali mengi✍️
By Hans Rafael