Web

Wamarekani Hawautaki Ushirikiano wa TRUMP na Elon Mask, Washambulia Magari ya Tesla

 

Wamarekani Hawautaki Ushirikiano wa TRUMP na Elon Mask, Washambulia Magari ya Tesla

Mashambulizi dhidi ya vituo vya Tesla yameongezeka baada ya #ElonMusk kushirikiana na utawala wa #Trump kwenye Idara ya Ufanisi wa Serikali (#DOGE), ambayo imepunguza matumizi makubwa ya serikali.


Miji kama Portland na Seattle imeathirika zaidi, huku magari ya Tesla, vituo vya kuchaji, na stoo za magari vikilengwa. Kwenye shambulio moja #LasVegas, magari kadhaa yaliwashwa moto na neno "#resist" likaandikwa kwenye jengo.


Mwanasheria Mkuu wa Marekani, Pam Bondi, alisema watu watatu waliokamatwa kwa mashambulizi hayo wanakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 kwa ugaidi wa ndani.


Trump alitumia #TruthSocial kutangaza kuwa wahusika wanapaswa kufungwa kwa miaka 20 na kupendekeza wafungwe katika magereza ya #ElSalvador, akiyataja mashambulizi hayo kama ugaidi wa ndani. Alisisitiza kuwa Tesla ni "kampuni kubwa ya Marekani" na hata kununua gari lake la #Tesla kuonyesha uungaji mkono.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad