Zari kudaiwa kodi karibia kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni moja kasoro je ni ule msemo wa mali za marehemu huwa zinaondokaga na mwenyewe unataka kujidhihirisha?
Inaripotiwa mfanyabiashara #ZariTheBossLady anadaiwa kodi na mamlaka ya huduma hiyo nchini Afrika Kusini SARS kiasi cha Rand milioni 5 takribani shilingi milioni 700 za Bongo.
Taarifa inaeleza awali Zari alikua anadaiwa Rand milioni 3 tu na alipewa barua ya onyo la mwisho agosti mwaka jana la kutakiwa alipe.
Lakini kutokana na kinachodaiwa ni yeye kutozingatia onyo hilo kodi ikajilimbikiza pamoja na faini hadi kufikia Rand milioni 5.1
Zari na mzazi mwenzie wa kwanza Ivan Ssemwanga walikua kivutio cha wengi mashariki na kusini mwa Afrika kutokana na maisha yao yaliyoonyesha wana utajiri mkubwa.
Ivan alifariki 2017
Source: Maimatha