Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika ametangaza rasmi kuwa hatashiriki kikao cha kusaini Kanuni ya Maadili ya Uchaguzi mwaka 2025 kitakachofanyika leo katika ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) jijini Dodoma.
Mnyika amesema yeye ndiye mwenye mamlaka kisheria ya kusaini maadili hayo kwa niaba ya chama, na hajamteua kiongozi wala afisa yeyote kushiriki au kuiwakilisha CHADEMA katika kikao hicho.