BREAKING: Rais Museveni atangazwa mshindi wa uchaguzi Uganda

Tume ya uchaguzi nchini Uganda imemtangaza Rais Yoweri Kaguta Museveni kama mshindi wa uchaguzi uliofanyika Alhamisi wiki hii, akiwa na jumla ya kura 7,946,772 ambayo ni asilimia 71.65% ya kura zote zilozopigwa.

Mpinzani wake wa karibu Robert Ssentamu Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine alikuwa wa pili, akiwa na jumla ya kura 2,741,238 au asilimia 24.72%.

Kwa mujibu wa tume hiyo, kura 11,366,201 zilipigwa katika uchaguzi huu wa mwaka 2026, ikiashiria asilimia 52.50% ya idadi ya wapiga kura waliojitokeza kushiriki.

Hata hivyo, kura 275,353 (2.42%) zilizopigwa zilikuwa batili.

Matokeo ya uchaguzi

Museveni 7,946,772 (71.65%)

Bobi Wine 2,741,238 (24.72%)

Bulira Frank 45,959 (0.41%)

Related Posts