
Mchezaji Seleman Mwalimu wa klabu ya Simba ya Dar es Salaam amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kumpiga kiwiko kwa makusudi mchezaji Andy Lobulka Bikoko wa Dodoma Jiji wakati mchezo tajwa hapo juu ukiendelea.
Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 41:5(5.2) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.
