
Serikali ya Senegal imetoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusu tuhuma za rushwa ndani ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) baada ya nchi hiyo kupokwa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 na kupewa Morocco.
Uamuzi wa CAF umetolewa baada ya bodi ya rufaa kueleza kuwa Senegal ilikiuka kanuni za mchezo wakati wa fainali ya michuano hiyo.
