Nature

Uchambuzi Mechi ya SIMBA na Gaborone, Kikubwa Simba Wamefuzu ila……

Gaborone walianza game vizuri sana na waliingia tofauti na mchezo wa kwanza “Suprise” ni vile walikosa usahihi wa maamuzi yao kwenye actions zao za mwisho …. Kivipi ?

1: Walipata urahisi wa kuivuka pressing wakiwa na watu watatu nyuma dhidi ya wawili wa Simba 3 vs 2 hapo wanapata rahisi kwao kufika eneo la mwisho .

2: Kwasababu Simba wanakuwa na space kubwa kati ya viungo na washambuliaji wao , Gaborone hawakuitaji ufanisi mkubwa wa pasi zao kuivuka pressing ya Simba na walipata space kwenye mpira wakati wa build up yao .

3: Wingers wa Simba ( Morice & Mpanzu) wanachelewa kutrack back kuwasaidia Fullbacks wao hapo inakuwa rahisi kwa Gaborone kutengeneza muunganiko mzuri pembeni ya kiwanja ( Combination Play ) rahisi kwa Gaborone kutengeneza mashambulizi yao kupitia pembeni .

4: Simba walikuwa wanapoteza pasi kirahisi hasa wakati wanaunda mashambulizi kuanzia eneo la chini ( Hakuna Connection ya pass zao kuanzia chini then wanakuwa na idadi ndogo ya wachezaji eneo la juu ) .

✍️ Nafikiri Gaborone walistahili kuimaliza game kipindi cha kwanza : walipata space kubwa wakati wanashambulia , wanafika kwenye eneo la mwisho kirahisi pia walikuwa na idadi nzuri ya wachezaji kwenye kiungo dhumuni ni kutengeneza combination play kwenye maeneo yote ( Pambeni na kwenye kiungo )

✍️ Gaborone United walikosa utulivu na maamuzi sahihi wakifika kwenye eneo la mwisho lakini kirahisi tu , wangekuwa na matumizi mazuri ya nafasi game ingemalizika kipindi cha kwanza .

NOTE :

1: Moussa Camara kafanya baadhi ya saves nzuri kuwaweka
Simba mchezoni

2: Ni kama Fitness level ya wachezaji wa Simba ipo chini sana ( ngumu kuwaona wakishinda mipambano yao kiwanjani ) .

3: Morice Abraham anacheza na haiba, anasimama na kuhesabiwa kama mmoja wa wachezaji viongozi

4: Kikubwa wamefuzu hatua inayofata, wanatakiwa kuboresha performance yao .

5: Umaliziaji wa kiwango cha chini kwa baadhi ya nafasi ulifanya mechi kuwa ya presha kwa Simba

FT: Simba 1-1 Gaborone Utd ( Agg 2-1)

By Kelvin Rabson

Related Posts