Nature

Al Ahly imerejea kileleni mwa Kundi B, Yanga ya Pili

Al Ahly imerejea kileleni mwa Kundi B kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) kufuatia sare ya 1-1 dhidi ya wenyeji, AS Far Rabat, wakifikisha alama 4 baada ya mechi mbili sawa na Young Africans Sc iliyoshuka mpaka nafasi ya pili.

AS FAR Rabat iliyopoteza 1-0 kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Wananchi ipo nafasi ya tatu alama moja baada ya mechi mbili huku JS Kablie iliyopoteza 4-1 dhidi ya Al Ahly kwenye mechi ya kwanza ikiburuza mkia alama moja baada ya mechi mbili.

Kwingineko, Mamelodi Sundowns imetoshana nguvu na MC Alger ya Algeria kwa sare tasa huku Sundowns ikikwea kileleni mwa Kundi C alama nne baada ya mechi mbili huku MC Alger ikiwa nafasi ya tatu alama moja baada ya mechi mbili.

FT: AS FAR Rabat πŸ‡²πŸ‡¦ 1-1 πŸ‡ͺπŸ‡¬ Al Ahly
⚽ 37’ Bouriga
⚽ 68’ Trezeguet

FT: MC Alger πŸ‡©πŸ‡Ώ 0-0 πŸ‡ΏπŸ‡¦ Mamelodi Sundowns

MSIMAMO KUNDI B

  1. πŸ‡ͺπŸ‡¬ Al Ahly β€” mechi 2β€” pointi 4
  2. πŸ‡ΉπŸ‡Ώ Yanga Sc β€” mechi 2β€” pointi 4
  3. FAR Rabat β€” mechi 2β€” pointi 1
  4. JS Kablie β€” mechi 2β€” pointi 1

Related Posts