
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Martha Mwaipaja amemjibu Mwimbaji mwenzie wa Nyimbo za Injili Upendo Nkone juu ya msamaha aliomuomba na kusema amekasirishwa zaidi na neno la ‘kutishiwa maisha’.
“Kinachomfanya aombe msamaha ni anaogopa sheria na sio kuiumiza nafsi yangu, kuna vitu viwili labda hapo nitatakakujua kwanini ananiomba msamaha….. sababu ameniumiza au ameogopa sheria? leo akipata matatizo nitasemaje, kwahiyo upendo aeleze vizuri nia yake ya kuomba msamaha kwasababu anaogopa au kwasababu amenifanyia unyama?’ —— Martha Mwaipaja.
Martha Mwaipaja anasema yote yaliyozungumzwa aliyapuuzia isipokuwa hilo la kumtishia maisha Upendo Nkone ambapo mahojiano haya yanapatikana kwa urefu kwenye Youtube
View this post on Instagram
