Nature

John Heche Apoi, Adai Hawaogopi Vitisho na Ukandamizaji Wanaopitia

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, John Heche, amesema kuwa chama hicho hakiogopi vitisho, ukandamizaji wala hila dhidi ya wapinzani, na kitaendelea kusimama kidete kutetea haki, uhuru na maisha ya Watanzania wote.

Akizungumza Julai 23, 2025, wakati wa kutoa salamu za chama katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Arumeru, Albert Elias Mollel, huko Ngaramtoni mkoani Arusha, Heche amesema kuwa taifa haliwezi kuendelea kwa viongozi wa umma kutumia mabavu kuwanyamazisha wanaowakosoa.

Aidha Heche ametoa matumaini kwa wanachama wa CHADEMA na Watanzania wote waliopoteza imani, akisema kuwa ushindi wa mabadiliko ni suala la muda tu.

Related Posts

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *