
Klabu ya Manchester United inajutia uamuzi wake wa kukubali kumuuza mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford kwa Barcelona kwa £26m kwa sababu wanaamini kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 sasa ana thamani ya takriban £50m. (Star)
Beki wa Bournemouth na Argentina Marcos Senesi, 28, anataka kujiunga na kalabu ya Barcelona msimu huu wa joto baada ya kuamua hatasaini mkataba mpya na Cherries. (Team Tal)
Mshambuliaji Muingereza Liam Delap, 23, huenda akaondoka Chelsea msimu huu wa joto, na hivyo kuzua shauku kutoka kwa vilabu vikiwemo Manchester United, Newcastle na Everton. (Caughtoffside)
