
Mdau unadhani Yanga wataendeleza dozi au Simba watakataa uteja?
Simba SC na Yanga SC wanatarajiwa kushuka dimbani Jumapili hii Machi 1, 2026 kwenye Uwanja wa Amaan Complex katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Mwamuzi wa kati anatarajiwa kuwa Nassoro Mwinchui akisaidiwa na Kassim Mpanga wa Dar es Salaam na Hamdani Said kutoka Mtwara huku Ramadhan Kayoko akiwa mwamuzi wa akiba.
