
Wananchi, Young Africans SC wamechomoza na ushindi mnono wa 3-0 dhidi ya Wajelajela, Tanzania Prisons katika dimba la KMC Complex na kuendelea kujitanua zaidi kileleni mwa msimamo wa Ligi kuu bara.
Wananchi wamefikisha alama 41 baada ya mechi 17 na kusogea mpaka alama 7 mbele ya mahasimu wao, Simba Sc waliopo nafasi ya pili ingawa Yanga SC imecheza mechi mbili zaidi.
FT: Yanga SC 3-0 TZ Prisons
⚽ 50’ Okello (🅰️ Mwenda
⚽ 68’ Mudathir (🅰️ Okello)
⚽ 86’ Pacome (🅰️ Abuya
