
Klabu za Young Africans na Simba zimetozwa faini ya Sh. 5,000,000 (milioni tano) kila moja kwa kosa la walinzi wake kugombana na kutoleana lugha ya matusi, jambo lililozua taharuki na kuchafua taswira ya mchezo huo wakati klabu ya Simba ikiwasili uwanjani hapo.
Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 47:1 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Klabu.
