
Taarifa kutoka nchini Libya ni kwamba Steven Desse Mukwala anakiwasha kweli kweli, ameanza vizuri akiwa na waajiri wake wapya Al Nasser akiwa amecheza mechi nne mpaka sasa na kufunga magoli matatu.
Mshambuliaji huyo raia wa Uganda, amejiunga na miamba hiyo ya Libya, akitokea klabu ya Simba Sc katika dirisha dogo la usajili.
Steven Mukwala, ambaye ni mshambuliaji mahiri na mwenye kipaji kikubwa cha kusakata boli anazidi kuonyesha ubora wake siku hadi siku.
