
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imemfungia kipa wa Yanga, Djigui Diarra michezo mitatu na kumtoza faini ya Tsh. Milioni 2 kwa kosa la kumshambulia Mwamuzi wa kati wa mchezo kati ya #MtibwaSugar dhidi ya Yanga mnamo Machi 21, 2026, kwa mujibu wa Kanuni ya 41:5(5.3) ya Ligi Kuu.
Pia, mchezaji huyo ametozwa faini ya Tsh. Milioni 2 nyingine kwa kosa la kuonesha kidole cha kati wakati akitoka uwanjani baada ya kumalizika kwa mchezo huo, kitendo kilichoashiria ishara ya matusi na dharau, kwa mujibu wa Kanuni ya 41:5(5.4) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Wachezaji.
