Messi Atangaza Kustaafu Timu ya Taifa Argentina Baada Ya Miaka 21

Messi Atangaza Kustaafu Timu ya Taifa Argentina Baada Ya Miaka 21
Messi Atangaza Kustaafu Timu ya Taifa Argentina Baada Ya Miaka 21

Taifa laArgentina, limepokea habari ya kushtua katika ulimwengu wa soka baada ya Lionel Messi kutangaza rasmi kustaafu timu ya taifa ya Argentina, akifunga ukurasa wa miaka 21 wa kuitumikia nchi yake. Messi ametangaza uamuzi huo kupitia ujumbe kwenye mitandao ya kijamii leo, Agosti 31, 2026.
Messi, mwenye umri wa miaka 39, amecheza mechi 207 akiwa na Argentina tangu alipocheza mechi yake ya kwanza mwaka 2005. Katika kipindi hicho, ameiongoza Argentina kushinda Kombe la Dunia 2022 pamoja na mataji mawili ya Copa América.

Amesema katika kipindi chote alichokuwa akichezea Argentina, alijitoa kwa moyo wote kwa ajili ya jezi hiyo, akilenga kuwapa furaha mashabiki na kuwafanya wajivunie kuwa Waargentina kupitia soka.
“Nimejitoa kila kitu, si katika miaka ya hivi karibuni ambayo tulishinda kila kitu, bali tangu mwanzo. Nilipambana na kujitoa kwa ajili ya jezi hii ili kuwapa furaha na kuwafanya mjivunie kuwa Waargentina kupitia soka,” amesema.

Mchezaji huyo amesema anajua kuwa hatua mbalimbali zinaanza kufungwa na kustaafu timu ya taifa ni moja ya hatua zinazomuumiza zaidi, akisisitiza kuwa ataendelea kuipenda Argentina licha ya kutokuwa sehemu ya kikosi.
Amesema amefikia hatua ambayo hana zaidi ya kutoa, huku akiamini kuwa kuna wachezaji vijana wenye uwezo mkubwa wanaokuja nyuma yake ambao wanastahili kupata nafasi katika timu ya taifa.
Pia amewashukuru mashabiki kwa upendo na sapoti waliompa kwa kipindi cha miaka 20, akisema atakikumbuka kwa hisia kubwa kipindi cha kuimba na kushangilia pamoja nao akiwa ndani ya uwanja.
Aidha, ametoa shukrani kwa familia yake, makocha, wachezaji wenzake na viongozi wote aliowahi kufanya nao kazi, akisema anabeba kumbukumbu na matukio yasiyosahaulika katika safari yake ya timu ya taifa.
Amesema anaondoka akiwa na amani na fahari kwa kuwa aliweza, pamoja na wachezaji wenzake, kuwapa mashabiki nyakati walizokuwa wakiziota.

Katika ujumbe huo, mchezaji huyo pia amesema maneno hayo aliyaandika Julai 21, siku mbili baada ya fainali, lakini baada ya kufariki kwa baba yake, amekuwa na uhakika zaidi kuhusu uamuzi wake wa kustaafu.
Amehitimisha ujumbe wake kwa kusema:
“Asante Mungu kwa kunifanya kuwa Muargentina. Vamos Argentina!”

Related Posts