
Polisi wa Uingereza wamemkamata Balozi wa zamani wa nchi hiyo mjini Washington Marekani, Peter Mandelson siku ya Jumatatu katika uchunguzi wa utovu wa nidhamu unaotokana na uhusiano wake na Jeffrey Epstein.
Jeshi la Polisi la Metropolitan la London lilisema maafisa wamemkamata Kiongozi huyo wa zamani wa miaka 72 kwa tuhuma za utovu wa nidhamu katika ofisi ya umma Kaskazini mwa London.
Jeshi hilo linachunguza madai kwamba Mwanasiasa huyo Mkuu wa Uingereza alivujisha mijadala ya ndani ya Serikali kwa mkosaji wa ngono aliyepatikana na hatia Jeffrey Epstein baada ya ajali ya kifedha ya 2008.
Barua pepe zilizotolewa kama sehemu ya faili za Epstein nchini Marekani zilionekana kumuonyesha Kiongozi huyo wakati huo akisambaza barua kwa Epstein, na hivyo kusababisha uchunguzi dhidi yake.
