Rais wa Marekani Donald Trump ameweka marufuku ya usafiri dhidi ya raia wa Tanzania katika vikwazo vya hivi karibuni vya usafiri.
Ikulu ya White House imesema vikwazo hivyo vinavyokusudia “kulinda usalama wa Marekani” vitaanza kutekelezwa Januari 1, 2026.
Katika amri ya rais ililotiwa saini Jumanne tarehe 16 Disemba, utawala wa Trump uliijumuisha Tanzania katika orodha ya nchi zinazokabiliwa na vikwazo vya muda vya kuingia Marekani, akitaja uzembe wa ukaguzi, uhakiki na upashanaji habari wa mamlaka ya Tanzania kuhusu raia wao.
Nchi nyingine za Afrika zinazokabiliwa na vikwazo hivyo ni Burkina Faso, Mali, Niger, Sudan Kusini, Syria pamoja na watu walio na pasipoti ya Mamlaka ya Palestina.
