Tajiri wa klabu ya Yanga Gharib Said Mohammed (GSM) ameahidi kutoa bilion 1 endapo klabu ya Yanga itafanikiwa kuwafunga As Far Rabat na kutinga hatua ya robo fainali siku ya leo.
Pesa hiyo imewekwa kwa lengo la kuwapa motisha wachezaji Yanga kuelekea mchezo wao wa ligi ya mabingwa Afrika utakaochezwa leo Februari 7 majira ya saa 4 usiku kwa saa za Afrika Masharika pale nchini Morocco.
