Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu (Kesi Na. 19605/2025), imeahirishwa katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam.
.
Ahirisho limetokana na upande wa Jamhuri kujibu pingamizi la mshitakiwa kuhusu Shahidi wa Siri, lililowasilishwa Novemba 2025.
.
Wakili wa Serikali, Nasorro Katuga, ameomba pingamizi hilo litupiliwe mbali kwa kukosa msingi. Mahakama itatoa uamuzi Jumatano, Februari 11, saa tatu asubuhi.
