
Shughuli pevu imemalizika katika dimba la Benjamin Mkapa kwenye Dabi ya Jiji la Dar es salaam, wenyeji, Azam FC wakitoshana nguvu kwa sare tasa dhidi ya Wananchi, Young Africans Sc kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara.
Wananchi wanaendelea kusalia kileleni alama 36 baada ya mechi 14 huku Wanalambalamba wakikwea mpaka nafasi ya pili alama 28 baada ya mechi 14.
FT: AZAM FC 0-0 YANGA SC
FT: Mbeya City 1-4 Singida Black Stars
