
Mchezaji David Kameta wa klabu ya Simba ametozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kuonekana akimwaga kimiminika kiwanjani wakati timu hiyo ilipozuru uwanja dakika chache baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Amaan, kitendo kilichotafsiriwa kama Imani za kishirikina.
Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 41:5(5.5) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.
