
Jana Machi 22, 2026 na leo Jumatatu, Machi 23, 2026, mabosi wa Yanga wamekuwa na muendelezo wa vikao ambavyo vinalenga kujadili mustakabali wa timu hiyo hasa wa miezi ya hivi karibuni.
Vikao hivyo huenda visimalizike vyema kwa benchi la ufundi la timu hiyo chini ya Mreno, Pedro Goncalves ambapo habari kutoka chanzo cha ndani ya timu hiyo, zinafichua kwamba huenda kuna vichwa vikaondolewa katika benchi hilo ili kupisha ujio wa wengine.
