Donald Trump “Sikuwapigia IRAN ili Tuzungumze, Wao Ndio Walionipigia”

Donald Trump "Sikuwapigia IRAN ili Tuzungumze, Wao Ndio Walionipigia"
Donald Trump “Sikuwapigia IRAN ili Tuzungumze, Wao Ndio Walionipigia”

Donald Trump “Sikuwapigia IRAN ili Tuzungumze, Wao Ndio Walionipigia”

Rais wa Marekani, Donald Trump, amefichua kuwa serikali ya Iran imetafuta mazungumzo ya dharura na utawala wake ili kuzuia shambulio kubwa la anga lililopangwa kuharibu kituo chao kikubwa cha kuzalisha umeme.

Akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuondoka Florida leo, Machi 23, 2026, Trump ameeleza kuwa mazungumzo hayo yamepiga hatua kubwa na pande zote mbili zimekaribia kukubaliana katika maeneo yote muhimu ili kusitisha mnyukano wa kijeshi Mashariki ya Kati.

Trump amedai kuwa jeshi la Marekani lilikuwa limepanga kulipua kituo kikubwa cha umeme nchini Iran kilichogharimu zaidi ya dola bilioni 10 kukijenga. Amesema kuwa tishio la shambulio hilo, ambalo lingeweza kukiharibu kituo hicho kwa “shuti moja”, ndilo lililopelekea viongozi wa Iran kupiga simu kuomba suluhu.

Rais Trump ameweka wazi kuwa sharti kuu la makubaliano yoyote ni Iran kuachana kabisa na mpango wake wa silaha za nyuklia. Ameongeza kuwa viongozi wa Iran tayari wamekubali sharti hilo, na Marekani iko tayari kwenda kuchukua urani iliyoratibiwa wao wenyewe ikiwa mkataba utafikiwa.

Akijibu swali kuhusu ni nani hasa anayezungumza naye nchini Iran baada ya Marekani kudai “kufuta” uongozi mwingi wa nchi hiyo katika awamu tatu za mashambulizi, Trump amesema wanashirikiana na “mtu wa ngazi ya juu” ambaye anaheshimika. Amekiri kuwa ni vigumu kupata viongozi wa kuzungumza nao kwa sasa kutokana na athari za vita vilivyopita.

Trump ameongeza kwa kusema kuwa ana matumaini makubwa kuwa suluhu itapatikana kwa sababu Iran wamechoka na hawataki kuona miundombinu yao iliyobaki ikiteketezwa.

Related Posts