
Waziri Patrobas Katambi Awaita Dudu Baya, Pipi Tida, Chidi Benz, Lokole na Noel
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi ametoa wito maalum kwa baadhi ya Wasanii maarufu mitandaoni kuhudhuria kikao maalum, huku ajenda za kikao hicho zikitarajiwa kuwekwa wazi kesho, Septemba 1, 2026.
Miongoni mwa Wasanii waliotajwa kuitwa katika kikao hicho ni Dudu Baya, Pipi Tida, Chidi Benz, Lokole na Noel pamoja na wengine, huku orodha ya walioitwa ikisomwa na Gigy Money na Dotto Magari.
Hadi sasa, ajenda rasmi za kikao hicho hazijawekwa wazi, ingawa majina ya baadhi ya walioitwa yameibua hisia kuwa huenda kikao hicho kikagusa masuala yanayohusu maadili na matumizi ya mitandao ya Kijamii.
ALSO READ | Niffer Aibua Mjadala Mitandaoni: Asema Hawezi Kuwa na Urafiki wa Karibu na Wanawake Wenzake

One thought on “Waziri Patrobas Katambi Awaita Dudu Baya, Pipi Tida, Chidi Benz, Lokole na Noel”
Comments are closed.