Shekhe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Kawambwa amesema kwamba alifungisha ndoa Diamond Platnumz na Zuchu miezi michache iliyopita.
Akizungumza na Mwanaspoti, Shekhe Walid amesema aliwafungisha ndoa hiyo wanamuziki hao miezi mitano iliyopita, lakini habari za kuachana hazifahamu.
Shekhe Warid hakutaka kuzungumzia hatua zilivyoanza hadi akatafutwa kuwafungisha ndoa Diamond na Zuchu na kwanini ilikuwa siri.

