
Azam FC iliyokuwa pungufu ya mchezaji mmoja baada ya Aishi Manula kuoneshwa kadi nyekundu imechomoza na ushindi wa 2-1 dhidi ya Wakusanya Mapato, TRA United katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Huu unakuwa ushindi wa kwanza kwa Wanalambalamba hao baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Polisi Tanzania kwenye mchezo wa ufunguzi huku TRA United ikishindwa kupata ushindi kwenye mchezo wa pili mfululizo baada ya sare kwenye mchezo wa ufunguzi.
FT: Azam FC 2-1 TRA United
⚽ 08’ Iddi Nado
⚽ 34’ Abdul Sopu
⚽ 46’ Kamisoko
🟥 77’ Manula
