
Fiston Mayele Atua Al Ahli Tripoli kwa Mkataba wa Miaka Miwili
Aliyekuwa mshambuliaji wa Yanga SC, Fiston Kalala Mayele, ametambulishwa rasmi kuwa mchezaji mpya wa klabu ya Al Ahli Tripoli ya nchini Libya, akitokea Pyramids FC ya Misri.
Nyota huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), mwenye umri wa miaka 32, amewasili klabuni hapo na kusaini mkataba wa miaka miwili. Mayele alipokelewa kwa furaha na umati mkubwa wa mashabiki wa Al Ahli Tripoli waliojitokeza kwenye viwanja vya klabu hiyo na kambini kumpa mapokezi ya kishujaa.
